Blog Details

YIA visits the Chinese Embassy in Tanzania

Images
Authored by
Joseph Mramba
Date Released
September 21, 2023
Comments
No Comments
Mkurugenzi na Mwanzilishi wa Taasisi ya Youth Investors Association @yia_tanzania Ndg. Joseph Mramba @official_mramba amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Jamhuri ya watu wa China anaewakilisha nchini Tanzania, Mheshimiwa Balozi, Chen Mingjian.

Huku dhumuni la kukutana ikiwa ni pamoja na kuzungumza ajenda mbalimbali zinazowahusu vijana, na kuelezea uzoefu wake wa uwakilishi wa vijana wa kitanzania kwenye mkutano wa kimataifa wa ushirikiano na maendeleo kwa wajasiriamali vijana. Ikiwa ni pamoja na uzinduzi wa Umoja wa Kimataifa wa Chama cha Wajasiriamali Vijana / International Alliance of Young Entrepreneurs Associations (IAYEA) uliofanyika beijing, china mwaka huu mwezi wa nne. Huku Taasisi ya Jumuiya ya Vijana Wawekezaji (YIA) @yia_tanzania likiwa ni miongoni mwa washirika kwenye mkutano huo pamoja na nchi nyingine 34.

Katika mazugumzo yao pia Ndg. Mramba ametafuta fursa za ushirikiano na ubalozi wa China kufanya kazi pamoja na Taasisi ya YIA katika kuleta maendeleo chanya katika maisha ya vijana kwa kuwawezesha na kuwainua vijana katika sekta mbalimbali. Naye Mheshimiwa Balozi, Chen Mingjian ameonesha nia ya kuunga mkono juhudi kubwa zinazo fanywa na vijana wadogo wa kitanzania kutoka kwenye Taasisi yao kwa kushirikiana katika programu na miradi yao mbalimbali.

Ndg. Mramba katika mkutano huu muhimu pia aliambatana na Mjumbe wa Bodi Dkt. Rajab Rutengwe pamoja na Meneja anaeshughulikia shughuli za taasisi Ndg. Cliff Mwangosi.

Share:

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Need help?

Call YIA Now

Youth Investors Association

YIA is where young entrepreneurs gather, grow, and turn big ideas into real impact. We empower, guide, and connect Tanzania’s youth to the tools, networks, and opportunities that shape the future.